Tuesday, March 22, 2016

Soudy Brown kampata Nyoshi kwenye U HEARD kuhusu uhusiano wa Maji na weupe wake.

Ikiwa leo March 22, 2015 Dunia inaadhimisha siku ya maji.. SOUDY BROWN ametuleta U HEARD kupitia XXL ya Clouds FM ambapo amemtafuta mwimbaji ambaye ni kiongozi wa bendi ya FM Academia ,Nyoshi El Sadaat kuzungumzia suala hilo.

“kwa siku mimi nakunywaga kama glasi ndogo tu, kwa siku hata mara sita au mara 10 kwa sababu ya joto, na ukiwa unakunywa maji mengi sana hata ngozi yako inakuwa vizuri, nyororo, maji yanasaidia sana kwenye mwili wa binadamu”- Nyoshi

Soud Brown:Hivi Ray Kigosi wa Bongo Movie unamjua hivi ngozi yake ni unavyoiona maji au vitu vingine?

Nyoshi..’Ni kutumia maji mengi na mazoezi tu yaani ukiwa unafanya mazoezi kisha unakunywa maji mengi utaona ngozi yako inakuwa imara kabisa inanyooka inakuwa nzuri, mimi situmii makopo muda wote kwasbabau inaweza ikaharibu ngozi kwa kawaida natumia maji kuwa msafi kuoga ngozi yangu inakuwa imara kabisa na wala si makopo‘- Nyoshi

No comments:

Post a Comment