Ukiachilia mbali aliposikika kwenye Like Father Like Son Remix ya msanii Stamina ni muda mrefu umepita hajasikika Noorah, huku wengi wakijiuliza nini sababu za ukimya wa msanii huyo.
Kupitia Planet Bongo ya East Africa Radio Noorah ameeleza kuwa ukimya wake ni kuhofia kutoa ngoma ambayo haitofanya vizuri, pia hapendi kukurupuka kutoa ngoma kuwepo mipango maalum kuhusu ngoma hiyo.
Noorah amesema kuna ngoma kadhaa kali aliwahi kuzitoa siku za nyuma lakini mipango ya promo haiku na kusababisha ngoma hizo kupotea kiaina jambo ambalo hataki litokee tena kwa ngoma zijazo.
Ameweka wazi kuwa zipo ngoma kibao ambazo amerekodi tayari lakini mipango ya Promo haijaridhisha kwahiyo anaona bora kukaa kimya kuliko kuzitoa hovyo zikapotea.
No comments:
Post a Comment