Katika maeneo yenye uhaba wa maji ya bomba, mvua ni chanzo muhimu sana cha maji ya kunywa katika ngazi ya kaya. Hivi karibuni msomaji wetu mmoja aliuliza; “Je, kuna tatizo lolote wanapata watu wanaotumia maji ya mvua kwa ajili ya kunywa?”
Kwa asili yake maji ya mvua kabla hayajafika katika anga letu huwa ni safi na salama kwa kunywa. Hata hivyo, maji hayo lazima yapite katika anga na ndipo yafike ardhini kama mvua.
Hapo ndipo hatari ya maji ya mvua inapoanza na kuongezeka zaidi yanapofika katika paa la nyumba au sehemu maalumu iliyojengwa kuvuna maji hayo na hatimaye kuhifadhiwa katika ndoo au tenki.
Maji ya mvua yanapopita katika anga hubeba vumbi, moshi na gesi mbalimbali zikiwamo carbon dioxide, oxygen, nitrogen dioxide na sulfur dioxide. Vitu hivyo hupunguza usafi na usalama wa maji ya mvua.
Uchafuzi zaidi wa maji ya mvua hutokea pale yanapofika katika paa la nyumba au sehemu maalumu iliyojengwa kuyavuna.
Maji ya mvua yanapofika katika paa au sehemu inayotumika kuyakusanya mara nyingi hubeba kemikali, vumbi, mchanga, vitu vilivyooza, majani, vinyesi vya ndege na wanyama.
Maji kama hayo yanapoingia katika chombo cha kuhifadhia yanaweza kuwa mazalia mazuri ya vijidudu vinavyosababisha magonjwa ya tumbo kama vile kuhara, homa ya tumbo, kipindupindu na hata kuzalisha mbu wanaoeneza magonjwa mbalimbali mfano malaria.
Tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa maji ya mvua mara tu baada ya kuvunwa huwa na vijidudu vinavyosababisha magonjwa ya tumbo, vikiwamo Giardia, Cryptosporidium, E. coli, Campylobacter, Vibrio, Salmonella, Shigella na Pseudomonas.
Maji ya mvua lazima yachemshwe kabla ya kuyatumia kwa kunywa au kupiga mswaki.
Idadi kubwa ya uchafu na vijidudu hupatikana pale mvua inapoanza kunyesha.
Watu wanashauriwa waanze kukinga au kuvuna maji dakika tano baada ya mvua kuanza kunyesha ili paa la nyumba au sehemu ingine inayotumika kukusanya maji ijisafishe kwa mvua ya kwanza.
Kwa kawaida, maji ya mvua hayana kiwango hatari cha kemikali zinazodhuru afya. Hata hivyo, mara nyingine kiwango cha kemikali ya zinc na lead huwa kikubwa kutokana na kuingia kemikali hizo kutoka katika paa la nyumba, tenki la kuhifadhia maji au angani.
Watu wanaovuna maji ya mvua kwa kiasi kikubwa, wanahimizwa kupima maji yao katika maabara za maji pale wanapoyavuna na miezi kadhaa baada ya kuyahifadhi.
Maji ya mvua yana uchachu na kiwango kidogo cha madini. Kiwango kidogo cha madini katika maji ya mvua kinayafanya maji hayo kukosa ladha ukilinganisha na maji ya kisima, mto, ziwa au bomba.
Kiasi kidogo cha madini kama calcium, magnesium, iron, na fluoride ni muhimu katika maji ili kuimarisha afya. Katika baadhi ya nchi, maji ya mvua husafishwa na kuongezwa madini muhimu kiafya na kusambazwa kwa wananchi kama maji ya kunywa.
Usafi na usalama wa maji ya mvua unategemea usafi wa paa la nyumba, gata, bomba na ndoo au tenki la kuhifadhia maji.
Wiki ijayo nitaelimisha juu ya namna bora na sahihi ya kuhifadhi maji ya mvua hasa katika matenki. Hii itasaidia sana jamii ya watu wa kipato cha chini ambao hutumia gharama kubwa kwa ajili ya kununua na kutumia muda mrefu wakitafuta maji.

Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.
ReplyDeleteMwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.
Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.
Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.
Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.
Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com
Uchawi wa mapenzi wa Dkt. Dawn hufanya maajabu kweli.
ReplyDeleteNiliwasiliana na Dkt. Dawn wakati uhusiano wangu ulipovunjika kabisa. Mpenzi wangu wa zamani alikuwa ameniacha na kunizuia kwenye mitandao yote ya kijamii. Nilivunjika moyo na kupoteza tumaini. Baada ya kushauriana na Dkt. Dawn, kila kitu kilibadilika. Mpenzi wangu wa zamani alirudi peke yake, akaomba msamaha kwa dhati, na akaomba msamaha. Leo, tunaishi pamoja kwa furaha, na hata tuna mtoto.
Maneno hayatoshi kuelezea jinsi ninavyoshukuru. Kutokana na uzoefu wangu, naweza kusema kwa ujasiri kwamba Dkt. Dawn ni halisi, anayetegemewa, na mwenye nguvu. Ikiwa unakabiliwa na hali yoyote ngumu maishani mwako hivi sasa, Dkt. Dawn anaweza kukusaidia.
ANAWEZA KUKUSAIDIA KWA MATATIZO YAFUATAYO:
Kurudisha ndoa na mahusiano yaliyovunjika
Kuvutia mafanikio na ukuaji katika biashara
Matatizo ya uanaume, utasa, na ukosefu wa watoto
Kurejesha mali zilizoibiwa au zilizopotea
Kurudisha kazi zilizopotea au fursa za kazi
Kinga dhidi ya uchawi na macho mabaya
Hirizi za mvuto
Kutatua migogoro ya ardhi na mali
Kuwafanya wapenzi kutimiza ahadi zao
Kushinda kesi mahakamani, na mengine mengi
Huu si ulaghai — ni ushuhuda kutoka kwa uzoefu.
Kwa maelezo zaidi, wasiliana naye moja kwa moja kwenye WhatsApp. +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com